Top Songs By Dizasta Vina
Similar Songs
Credits
AUSFÜHRENDE KÜNSTLER:INNEN
Dizasta Vina
Künstler:in
KOMPOSITION UND LIEDTEXT
Edger Vicent mwaipeta
Songwriter:in
Lyrics
Ah...
Nakusalimu mwafrika...nakusalimu habari gani.../
Nikaribishe tuketi...niseme yaliyo ndani.../
Sahau kuhusu hadithi za kale...za upendo wako.../
Nataka leo tukae...tuijadili kesho yako.../
Kutoka kupiga ramli...na kutii mizimu.../
Umeanza kufata amri...za TV na simu.../
Na ubaya ni kwamba...umeanza kuikacha sanaa.../
Na kufata siasa...ambayo inakulaza na njaa.../
Na kila unachokiona...unataka kubeba.../
Vichache vimekushinda...na unapanga kuongeza.../
Juzuu,Katekisimu mpaka Novena.../
Sio zako...zako zilikuwa ni kutamba ngojera.../
Umezubaa...majirani wameanza kufika kwako.../
Na unaamini kuwa...watakubebea shida zako.../
Kwa sababu ya ujinga,umezidi umasikini.../
Unamjengea jirani...kwako unachimba unabaki chini.../
Zamani...ulikuwa una sembe ya kusaza.../
Uliabudu kazi...ukaliweka jembe kwenye shamba.../
Ghafla ukauza panga...ukapamba jembe kwenye kabati.../
Ukanunua kioo ujirembe...ili uende na wakati.../
Ume...chagua urembo na umetupa werevu.../
Umeuza mifugo...unafuga kucha na ndevu.../
Familia iwe...mwafrika uzame mitini.../
Au uombe msaada..wakati unakufa na fasheni mwilini.../
Mwafrika..una mzigo mkubwa wa madeni.../
Hauna mali ..ardhi yako ni 'future ya wageni.../
Unalala ndani...kungoja hisani ya wenye nguvu.../
Nyumba iko wazi..wewe uko ibadani unaabudu.../
Ujasili ni kujimudu...mwafrika haujui hili.../
Umejaliwa nguvu...na unashindwa kuzihimili.../
Unavamia diplomasia..unatunga hotuba.../
Na hakuna mwenye hisia...kuwa upo nyuma ya muda.../
Ah..
Unapoteza stadi za maisha.../
Kwa elimu ya magharibi...ikuweke ofisini suti kubwa..
Ukumbatie dawati la nyazifa.../
Huku unauwa..nguvu kazi ya taifa.../
Umepitiliza nyumbani...hauna vituo.../
Umekuwa mtumwa wa sera zao,kiasi kwamba hauna 'future..
Hauna dira,hauna lugha hauna nguo.../
Milango ya fahamu..imefungwa na ufunguo.../
Umepewa karatasi...ukaita jina pesa.../
Ukasubiri ikuletee furaha..ikakutesa.../
Ukauza umoja...ukauza amani ukauza utu.../
Ukawashusha mashujaa wako..ukamwinua Yesu wa kizungu.../
Una kucha ndefu ..kushika chungu matusi.../
Hauwezi kuandika history..haumudu herufi.../
Ume-bleech nywele,mdomo mwekundu umebusu baruti.../
Nikuite nani...mwafrika mzungu au mzungu mweusi.../
Ah..
Unadanganywa...rangi yako sio nzuri.../
Ili utafute pesa...ukawaungishe vipuri.../
Ume-switch kutoka Mama Afrika...mpaka drama Queen.../
Una nunua TV...uone Afrika ikizama chini...!/
Mwafrika..umeshakosa mipango.../
Unajua kuchonga ngenga..badala ya kuchonga vinyago.../
Unaacha wanyama Mikumi,Serengeti unasafiri.. unaenda kushangaa ghorofa Chicago.../
Unarudi..unajikuta Mmarekani eti real ****...!/
Mbona haulili bili ****...?/
Jasiri..haiachi asili real ****.../
Kamwe usijiite G ****.../
Hauwezi kuwa warrior../
Unajua majina ya wasanii..kishinda historia.../
Unasahu mapishi..hauendi jikoni.../
Unakufa na ngoma mwilini...cheni shingoni.../
Kwa heshima na taadhima...unautunza Msaafu.../
Unatupa kitenge..kisha unafunga hijabu.../
Na ubaya ni kwamba...bado haujajua sababu.../
Unapewa Zaburi..utafakari mwenyewe wakichukua dhahabu.../
Ufeli majibu...uishie kubuni.../
Ushindane nani msafi...aende mbinguni.../
Mhanga wewe...rudi uzipitie kanuni.../
Umeshikishwa kitabu...wenzio wakushikie uchumi.../
Mwafrika...hii haikuingii nikichana.../
Unanuka sana...kiasi hauvutii kama Jana.../
Kiburi moyoni..haisikii unapokanywa.../
Unatia aibu..kiukweli sijivunii kuwa mwana.../
Na bado unaamini..shahada ya shule ni zana.../
Haujui...ukitaka ule ni shamba.../
Unafunga ubongo...unafungua mikono ili wakupe msaada.../
Umesahau kuwa...vya bure gharama.../
Mchezo wako...sheria zao utashindwa.../
Ukiishi porini..kama haiwindi..utawindwa.../
Inasikitisha..wenzako wanaigiza ili waishi...ila we unaishi kwa kuigiza sio...?/
Umekuwa dekio..umekubali kuwa soko la pombe
Na sigara.../
Soko la risasi bunduki na mabomu...
Soko la madawa ya kulevya..yanauwa waafrika wenzio.../
Soko LA dini zao..soko la picha za uchi .../
Soko la vitukukuziba sauti.../
Soko la sera unevu..na mifumo gombanishi...
Magonjwa batiri..unanunua dawa kwa kuhisi sio...?/
Umezagaa visingizio.../
Haujui akiba..ndio maana unashangaa salio.../
Umegeuzwa kifaa cha majaribio.../
Imeandikwa..asiyeandaa silaha ataandaa mapambio.../
Mwafrika...
Nakupa nahau kalili.../
Afrika inakufa..mwafrika unadharau dalili.../
Unasahau wito..unafata mkumbo kwa dau batili.../
Unakumbuka kila kitu..na unasahau asili.../
Written by: Edger Vicent mwaipeta